Huenda usalama katika kaunti ya Mombasa ukaimarika baada ya
serikali ya kaunti hiyo ,kutoa zabuni ya kununua mashini za kubaini vilipuzi
,mashine zinazojulikana kwa lugha ya kimombo “explosive trace and vapour
detector”….
Katibu wa biashara kaunti ya Mombasa Mohammed Abdi amebaini
kuwa mashini hizo zitakuwa na uwezo wa kujua iwapo kuna vilipuzi ama hata
mabaki ya vilipuzi, na zitaweza kutumika katika maeneo yenye watu wengi ikiwemo
eneo la Fery,soko la Kongowea na hata afisi zenye watu wengi.
Abdi amesema kuwa mashini hizo huenda zikapunguza masuala ya ukosefu wa usalama
katika kaunti hiyo.
Hatua hii imepokelewa vyema na wafanyi biashara katika soko
hilo wakisema kuwa huenda visa vya ukosefu wa usalama ambayvo vimekuwa vikishuhudiwa ndani ya soko
hilo vikapungua.
Kauli hizi zinajiri baada ya kushuhudiwa ukosefu wa usalama
ndani ya kaunti ya Mombasa,ikiwa kisa cha hivi punde zaidi ni kupigwa
risasi kwa afisa mmoja wa kitengo cha
upelelezi katika eneo la Bakarani na kufariki.
No comments:
Post a Comment