Saturday, July 26, 2014

KEMNAC



 Viongozi wa dini na wahubiri wa makanisa mbalimbali katika gatuzi dogo la Likoni kaunti ya Mombasa, wamesisitiza umoja  miongoni mwa wakazi wa eneo hilo mbali na pia kuonyesha ushirikiano na idara ya usalama ili kukabilina na visa vya kihalifu ambavyo vimekuwa vikishuhudiwa katika siku chache zilizopita.

Wakizungumza na waandishi wa habari katika kanisa la Jcc huko Likoni,Joseph Maisha wa kanisa la Redeemed amesisitiza umuhimu wa kushi kwa amani na huku akiwataka wakazi wa eneo hilo wasigawanywe kwa misingi ya kikabila na dini.Maisha ameongeza kuwa huenda ikawa ni ajenda za watu ambao wana malengo ya kuwagawanya wakazi hao ambao wameishi hasa baada ya pia kushuhudiwa na vikaratasi ambavyo vimekuwa vikiangushwa na kutia hamasa miongini mwa jamii fulani.

Wakati huo mhubiri wa dini ya kiisilamu ambaye pia ni mshirikishi katika baraza la kiisilamu na ushauri nchini KEMNAC Maalimu Sineno kutoka aneo la Mtongwe amesema kuwa kwa muda watu wamekuwa wakishi kama ndugu na ina sikitisha kuona kuwa mambo kama hayo yanashuhudiwa katika eneo hilo ila pia akahidi kuwa viongozi wa dini wanafnya kila la msingi kushauri waumini na vijana kutojihusisha na visa kama hivyo.

No comments:

Post a Comment