Saturday, July 26, 2014

UCHAGUZI



GAVANA WA MOMBASA HASSAN JOHO
 Baadhi ya wawakilishi wa bunge la kaunti ya Mombasa kutoka mrengo wa ODM wamefanya mkutano mapema hii leo wakuchagua mwakilishi wa walio wengi bungeni.hii ni baada ya wawakilishi hao kupitisha kura ya kutokua na imani kwa aliyekua kiongozi wao Khamis mwabashiri.

Abdallah Kasagamba kutoka likoni alichaguliwa kuwa kiongozi wa wengi katika bunge hilo.Duru za kuaminika kutoka kikosi cha gavana wa Mombasa Hassan joho zinasema kuwa uchaguzi wa kasagamba ni kutayarisha vijana kisiasa ili waweze kuchukua nafasi ya mbunge  Masud mwahima ambaye amekuwa kiongozi kwa mda mrefu sasa.   

Duru hizo zimeongeza kuwa uchaguzi wa Afya Rama kama mwenyekiti wakikundi cha maendeleo ya wanawake ni katika hali ya kumtayarisha kuwania kiti cha ubenge cha mvita nafasi ambayo imeshikiliwa na Abdulswamad Nassir kutoka ODM ambaye pia amejitoa kwenye kikosi cha joho.Rashid Benzimba wa chama cha ODM ambaye alikua rafiki wa karibu wa joho naye pia amejitoa kwenye kikosi hicho.

Kutokana na baadhi ya viongozi kutoka kaunti ya Mombasa tuliyofanikiwa kuongea nao wamesema kuwa sababu kuu ya wawakilishi hao kumuondoa mwabashiri ni kutofaulu kupitisha miswada ya chama chao bungeni.

No comments:

Post a Comment