Saturday, July 26, 2014

MARIKITI



Huku mwezi mtukufu wa ramadhan ukiwa katika kumi lake la mwisho, wafanyibiashara katika soko la Marikiti ndipo wanapozidi kunogewa na biashara .

Wafanyi biashara hao wamesema kuwa mwezi huu huwa muhimu kwao kwani biashara huimarika ijapokuwa Suala la ukosefu wa usalama limeonekana kutia hofu watu wengi ,kutokana na mashambulizi ambayo yamekuwa yakishuhudiwa eneo la pwani.

 Aidha wamebaini kuwa wengi wa waumini wa dini ya kiislamu wako mbioni kununulia jamaa zao mavazi, lakini wamesisitiza kuwa ni sharti usalama uimarishwe kwani idadi ya wale wanaozuru maduka hayo wakati wa usiku imepungua ,ikilinganishwa na msimu sawia na huu mwaka uliopita.

No comments:

Post a Comment