Serikali bado inafanya mazungumzo na Waitiki
anaye daiwa kuwa mmliki wa ardhi ya zaidi ya ekari mia tisa katika eneo kubwa
la likoni lifaamikalo kama magwagwani. Haya yalijiri baada ya waitiki kupeleka
kibali cha kumiliki adhi hiyo mara ya pili mahakamani.
Kamishna wa polisi
kaunti ya Mombasa Nelson Marwa
alipokuwa akiwahutubia wananchi waliokuwa wamejawa na ghadhabu baada ya
mahakama kutoa amri ya kuwataka kaaji
waeneo hilo kuhama. Marwa amesema kuwa mtu yeyote anayeishi katika sehemu hiyo
kutokuwa na hofu.
Vilevile mbunge wa Likoni Masoud Mwahima aliunga mkono
kauli ya Marwa na kusistiza akadai
waitiki kutohangaisha wakaaji bali kushirikiana na serikali kupata suluhisho .
Inadaiwa kuwa zaidi ya wananchi laki mbili na nusu wanaishi katika ardhi ya
Waitiki huku zaidi ya nyumba laki moja na nusu zikiwa zimejengwa.
No comments:
Post a Comment