Saturday, July 26, 2014

USAFIRI




 
Serikali ya kaunti ya Mombasa  ina mipango kabambe ya kuanzisha vituo vya abiria kuabiri magari katikati ya mji na vitongoji vyake kama njia moja ya kupunguza msongamano wa magari hiyo.

Haya ni kulingana na mwakilishi wa wadi ya Changamwe Jimmy Odari,ambaye ameeleza kuwa ili kupunguza na kumaliza kabisa msongamano wa magari unaoshuhudiwa kila mara katika barabara za kaunti ni lazima kuweko na vituo maalum vya kupandia magari.

Mwakilishi huyo amesema kuwa vituo hivyo vitahusisha matatu,piki piki na tuk tuk.

Aidha amedokeza kuwa hiyo ndio njia pekee itakayosaidia kaunti ya Mombasa kuwa na usafiri wa haraka,akisema kuwa upakiaji na kushukisha abiria kiholela kumechangia pakubwa kwa msangamano wa magari.

Huenda hatua hii ya kutengea matatu vituo vya kubeba abiria ikaleta afueni kwa madereva wa matatu kwani mara nyingi wamekuwa wakilalama kuwa wanasumbuliwa na maafisa wa traffiki kwa kuegesha gari mahali ambapo hapastahili.














 


No comments:

Post a Comment